Friday, November 20, 2009

JK awachana TFF....!!

Rais Jakaya Kikwete 'JK' akiteta jambo na mmoja wa viongozi wa kampuni ya Cocacola waliodhamini ziara ya Kombe la dunia hapa Tanzania 2009, kabla ya kutoa hotuba fupi iliyojaa makavu kwa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF).

President amefikisha kilio cha wadau wengi walioshindwa kuwaambia ukweli majamaa wa TFF ambao wako madarakani na hakuna mazuri yoyote wanayofanya kuhakikisha soka la bongo linakuwa siku hadi siku.

Makavu yao ndio wameshapewa, hivyo ni kazi kwa TFF kurekebisha walipokosea na kulisongesha soka la Bongo kwa kwenda mbele, sio kuendekeza timu kubwa na kutoa adhabu ambazo zinadidimiza viwango vya wachezaji na mpango mzima wa mpira Tanzania.......

Bado Maximo sasa, km vp asepe tu.......!



No comments:

Post a Comment