Tuesday, October 6, 2009

Mjomba Mjomba mgeni uzinduzi wa 'Mayrose Tv Talk Show' Oktoba 9!!

Mrisho Mpoto msanii wa muziki wa kizazi kipya, atakuwa mgeni katika uzinduzi wa kipindi cha 'Mayrose Tv Talk Show', utakaofanyika Oktoba 9 ktk Ukumbi wa PTA, Sabasaba, Dar es Salaam.

Kipindi hicho kitarushwa moja kwa moja ktk Televisheni ya Star Tv kikiwa kinaelezea masuala mbalimbali ya jamii,yahusuyo elimu na maisha kwa ujumla.

Akizungumza jijini Mwenyekiti mtendaji wa Shirika la maendeleo ya jamii, Mayrose Kavura amesema Sambamba na Mpoto pia atakuwepo Mmiliki wa Global Publication, Eric Shigongo, ambao watashiriki kutoa mada mbalimbali wakiwa mfano kwa jamii.

Bi.Kavura alisema, baada ya uzinduzi, kipindi hicho kiteandela kurushwa na kituo hicho kila siku ya jumapili kikirikodiwa kabla ya kurushwa hewani.

No comments:

Post a Comment