Friday, February 26, 2010

Sheikhe Yahaya awatisha watakaogombea Urais na Rais JK

HII NI PICHA YA JINI LITAKALO MTOA ROHO ATAKAYE SHINDANA NA RAIS J.K KIKWETE

Kauli za mtabiri maarufu wa nyota Afrika Mashariki na Kati Sheikh Yahya Hussein zimeonekana kuwatia hofu kubwa wagombea mbalimbali wa Uraisi nchini Tanzania ktk Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu mwishoni.

Hivi karibuni Sheikh Yahya Husein alitabiri kuwa , yeyote atakayejitokeza kuwania nafasi ya urais kumpinga Rais Jakaya Kikwete kuwania nafasi ya urais ndani ya chama chake atakufa ghafla.

Kauli hiyo ilionekana kuwagusa viongozi mbalimbali na wanachama ndani ya CCM ambao walijitokeza kutoa maoni yao mbalimbali.

No comments:

Post a Comment