Tuesday, November 27, 2012

R.I.P SHARO MILIONEA

 Msanii/Muigizaji/Mchekeshaji Hussein Ramadhani Mtioeti (27) maarufu SHARO MILIONEA amefariki dunia katika ajali ya gari jijini Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Prudence Masawe, amethibitisha kutokea kwa ajali na kusema kuwa marehemu amefikwa na umauti baada ya gari lake aina ya Toyota Haria lenye namba za usajili T478DVR kuacha njia na kupinduka.

Kamanda Massawe amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa mbili usiku wa Novemba 26, 2012 katika kijiji cha Maguzoni Soga Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.

Akisimulia zaidi RPC Massawe anasema kuwa marehemu alikuwa akiendesha gari hilo na alikuwa peke yake bila abiria mwingine na ajali kumfika akiwa katika kijiji hicho kilichopo kati ya segera na Muheza.

“Marehemu ndie alikuwa akiendesha gari lile, na lililopopinduika yeye alirushwa nje lkupitia kiooo cha mbele na umauti kumfika hapo hapo” alisema Kamanda Massawe.

Aidha Kamanda Massawe amesema msanii huyo alikuwa akitokea jijini Dar es Salaam na alikuwa akienda nyumbani kwao Muheza.
 
BLOG YA MAKAVU INATOA POLE KWA NDUGU JAMAA NA WADAU WOTE WALIOFIKWA NA MAJONZI

HAKIKA KILA NAFSI ITAONJA MAUTI

No comments:

Post a Comment