Tuesday, April 16, 2013

'MON G' Aziba Pengo la 'Q JAY'

 
Mkali wa RnB aliyekuwa akiwakilisha Wakali Kwanza Joseph Mapunda aka 'Q JAY' aliamua kuachana na Muziki wa kizazi kipya mara baada ya kuokoka na kuoa takribani miaka mitatu nyuma, sasa ni kama Pengo lake la Ukali wa RnB Bongo limezibwa na msanii Ally Ramadhan aka MON G....... 

Wakiitambulisha Ngoma mpya ya Mon G ft. Pthe MC inayoitwa "Badilika" jumamosi iliyopita ktk kipindi cha Bongofleva redioni chini ya Presenter mahiri Adam Mchomvu aka 'Baba Jonii' baadhi ya wadau wa BongoFlava walithihirisha hilo na kumpa BigUp kubwa msanii Mon G huku wakimlinganisha sawa na Q Jay aliyekuwa anafanya style hiyo ya muziki siku za nyuma!

MON G, mpaka sasa ameshaachia nyimbo kadhaa zikiwemo; Damu yangu, Mtoto wa Dar, Uko wapi, Na wewe pamoja na Badilika. Zote zipo hapa chini......ENJOY!
 

No comments:

Post a Comment