Thursday, November 28, 2013

Fainali ya EBSS Jumamosi hii.......

Katika kuelekea Fainali ya EBSS 2013 kesho kutakuwa na Press Conference pale katika ufukwe wa ESCAPE ONE  Saa Tano Asubuhi, ambapo utawaona washiriki wote walioingia Fainali kwa pamoja kabla ya siku yenyewe ya Jumamosi tarehe 30 ambapo wote kwa pamoja tutashuhudia Yule Mshindi wa Milioni 50.

Waliofanikiwa kuingia fainali ni Amina Chibaba (MBEYA), Melisa John (DSM), Elizabeth Mwakijambile (DSM), Emannuel Msuya (MWANZA) na Maina Thadei (DSM)

Pia siku ya Fainali kutakuwa na Burudani kutoka kwa Snura, Barnaba, Young Killer, Shaa, Walter Chilambo, Peter Msechu  na Makomandoo

Kiingilio katika Fainali hizo kitakuwa : VIP TSH 50,000/= KAWAIDA  : TSH 20,000/=

Tiketi  za siku ya Fainali zinapatikana sehemu zifuatazo :
-          Shear illusion
-          Biggy Respect (Kariakoo)
-          Steers Mjini
-          Zizzoue Fashion (Victoria na Sinza)
-          Photo Point (Mayfair)
-          Robby One Fashion (Kinondoni)
-          Best Bite
-          Engen Mbezi
-          Escape One (Mikocheni)
-          Benchmark Office Mikocheni
-          American Nails (Kinondoni)

No comments:

Post a Comment