Wednesday, March 4, 2015

NGOMA AFRICA BAND KUTUMBUIZA LIVE MJINI STUTTGART ,GERMANY

 
                 Africa Unite Party   Jumamosi 14 March 2015

Bendi ya maarufu Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni aka Anunaki aliens 
bendi hiyo inatarajiwa kutumbuiza katika onyesho maalumu la AFRICA UNITE PARTY litakalofanyika katika ukumbi wa VTS uliopo mtaa wa Augusburger Str.442 D-70327 mjini Stuttgart,nchini Ujerumani.Onyesho hilo limeandaliwa
na shirika la Afrikaktiv e.V wakishirikiana na  shirika la Cabaret du Monde,
Ngoma Africa band iliyozoeleka kwa kuwatia kiwewe washabiki wake kila
kona duniani wataporomosha muziki moto moto na mdundo wao maarafu
kama " Extraordinary Bongo Dansi" mdundo unaotingisha bila ya kuwa na
mpinzani huko ughaibuni, bendi hiyo inadumu katika medani ya muziki kwa
muda wa miaka 23 na kufanikiwa kujizolea washabiki kila kona.
Ticket za onyesho hilo zinapatikana kwa simu ( booking): Call9+49 0)152 12091242 au +49(0)152 106106137 Mnakaribishwa wote,pia usikose kuwasikiliza
FFU-Ughaibuni at www.ngoma-africa.com

No comments:

Post a Comment