FFU Kulitingisha hekalu la UEBERSEE MUSEUM-Bremen,Ujerumani siku 30 May 2015
Bendi
maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band almaarufu
kama FFU-Ughaibuni yenye maskani yeke nchini Ujerumani,siku ya jumamosi
30 Mei 2015 bendi hiyo italitingisha hekalu la Uebersee Museum mjini
Bremen,kuanzia Saa moja Usiku hadi kumekucha.
Onyesho hilo la usiku
usiokwisha limeandaliwa na utawala wa hekalu hilo la makumbusho la
Uebersee Museum,ambapo utawala huo umeiomba bendi ya Ngoma Africa band
kwenda kutumbuiza,kwa kuwa bendi hiyo ilitumbuiza mwaka 2013 na kuvunja
rekodi ya kuwavuta washabiki wengi kuliko bendi yeyote katika historia
ya matamasha yafanyikao katika hekalu hilo.
Ngoma Africa band
inayoongozwa na kamanda Ras Makunja ni bendi pekee ya kiafrika yenye
mvuto mkubwa barani ulaya,na washabiki wake wameipachika majina mengi ya
kiusanii kama vile FFU-Ughaibuni,Viumbe wa ajabu ANUNNAKI Alien's
(himaya ya mazimwi wa Anunnaki), pia maarufu kwa majina kama Mzimu wa
Muziki,na "Watoto wa Mbwa" .
Ngoma Africa band pia inatajiri wa
wanamuziki wenye vipaji vya hali ya juu wakiwemo yule mpiga solo mahiri
Afande Chris Bakottesa aka Afande Chris-B, Sanjint major Jo jo Sousa,
wanamuziki chipukizi wengi walizalishwa na bendi hiyo ambayo
inawanamuziki kumi.
Ngoma Africa band ilianzishwa mwaka 1993
na kiongozi wa bendi hiyo ambaye pia ni mtunzi wa nyimbo nyingi za bendi
hiyo Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja.
unaweza kuwasikiiza FFU
No comments:
Post a Comment