Friday, September 25, 2009

Twanga Pepeta kupiga nyimbo mpya Mango Garden Kesho....... Extra Bongo ya Ali Choki yamnyemelea star wake!!

Wanamuziki wa bendi ya African Stars Janeth Isinike (kushoto) na Saulo John (Ferguson) wakiimba kwa pamoja kwenye ukumbi wa Mango Garden Dar es Salaam, kesho watakuwepo tena watakapopiga nyimbo kutoka ktk albamu yao mpya.



Baada ya kuwarusha vilivyo ktk sikukuu ya IDD km kawaida kikosi cha bendi maarufu ya African Stars 'Twanga Pepeta' itakuwepo tena ktk ukumbi tulivu wa MANGO Garden uliopo Kinondoni kutoa burudani kwa wapenzi wa muziki itakapotambulisha nyimbo mpya katika albamu yao mpya ya Mwana Dar es Salaam.


Baadhi ya wanamuziki wa African stars 'Twanga Pepeta'

Pia kuna mazungumzo ya chini kwa chini juu ya wapenzi wa Extra Bongo kuwamezea mate wanamuziki wakali (ma-star) wanaopiga mzigo ktk bendi ya 'Twanga' wakipenda kuona wanaamia kunako bendi yao...!! Tusubiri tuone mdau, lisemwalo si lipo! Au......???!

No comments:

Post a Comment