Thursday, October 29, 2009

Baada ya kupagawisha mikoani, Fiesta kushuka na BUSTA shoo ya Dar Nov. 7.......!

Mkali wa hiphop nchini Marekani Trevor Tahiem Smith aka 'Busta Ryhmes' anatarajiwa kutua jijini kwa ajili ya shoo kubwa iliyoanzia mikoani ambayo mwaka huu imepewa jina la 'Fiesta One Love'. Tamasha hilo kubwa ambalo huandaliwa na kituo cha Radio Clouds FM kila mwaka chini ya Mkurugenzi wa kituo hicho Joseph Kusaga alisema Busta Ryhmes atatua tayari kwa onyesho hilo linalotarajiwa kufanyika tarehe 7 mwezi ujao.

Alikuwa na mtangazaji wa kipindi cha Power Breakfast Babra aliyeamka na hisia za
kupiga nyimbo za Busta toka mwanzo wa show mpaka pale mtangazaji mwenzake
Gerald Hando kumuuliza imekuwaje leo aamke na nyimbo za mkali huyo toka kwenye
kundi la Flip Mode na ndipo alipojibu ya kuwa anahisi kama Busta atakuwa jijini
kwenye onyesho hilo, ndipo walipompigia simu Mkurugenzi wao na kulithibitisha hilo.

Busta ambaye ana album tano anatamba na nyimbo kama Dangerous, Gimme Some More and Woo Hah! Pass the Courvoisier, As i come back, na nyingine nyingi anatarajiwa kuangusha bonge la shoo pale Leaderz jijini Dsm.

No comments:

Post a Comment