Tuesday, October 20, 2009

Leonel awakaanga Elizabeth na Kelvin Bigbrother...!!


Eliza kulia akiwa na Keli mwanamuziki wa USA alipoenda kuwatumbiza jumbani wiki iliyopita

Mapema Usiku wa kuamkia leo mwakilishi wa Tanzania na mshirika wake Kevin kutoka Nigeria walidumbukizwa ktk msala wa kutolewa ktk jumba la mashindano ya Bigbrother yanayoendelea baada ya kiongozi wa jumba hilo kwa wiki hii kuwachomeka wao akijiokoa ye mwenyewe na mshirika wake Mzamo kutoka Malawi.



Eliza na Kevin

Ktk kura zao binafsi za nani atoke Elizabeth na mwenzake walipigiwa kura moja tu na wenzao, ila kwa nguvu aliyonayo Head of tha House kwa wiki hii Leonel aliwataja wao ili wapigiwe kura na mataifa ya Afrika kutoka jumbani humo. Wengine wanaopigiwa ni Kristal wa Zimbabwe na Quinn wa South Africa, kati ya couple hizi 2 watakaopigiwa kura chache za kubaki na waAfrika watayaaga mashindano hayo matamu yaliyotutoa kimasomaso mwaka juzi kupitia kwa Richard.


Wadau tumpigie kura mwakilishi wetu Elizabeth na Kevin, aendelee kupeperusha bendera yetu vyema. MUNGU MBARIKI ELIZABETH.... MUNGU BARIKI TANZANIA....!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment