Tuesday, November 3, 2009

Mnamibia 'Eddy' alipiza kisasi kwa Mtanzania 'Eliza' atoke Bigbrother...!


Wakiwa wamebaki 9 ndani ya jumba Na kuongezewa mbwa anayeitwa 'Ruby' usiku wa kuamkia leo ili awape kampan, jana washiriki walipigiana tena kura za kutoka ambapo Mzamo, Emma na Nkenna walipata kura nyingi kuliko wengine.
Edward ambaye ndie kiongozi wa jumba kwa wiki hii aliitwa na Bigbrother ili amuokeo mmoja na kum-replace mwingine, Eddy alionyesha kweli anataka kulipiza kisasi kwa dada yetu Mtanzania Elizabeth kwani ktk kura za awali alipata kura 2 ikiwemo ya kwake na kunusurika kuwamo kikaangoni lakini Edward akamuingiza tena kwa kumuokoa Mzamo na kum-reprlace yeye, kisasi cha Eliza kumtoa pacha wake Erustus wakati alipokuwa HoH wiki za mwanzoni.



Pamoja na Eliza wengine walioingia kwenye msala huo ni Emma wa Angola na Nkenna wa Nigeria, MDAU USISAHAU KUMPIGIA KURA ELIZABETH AENDELEE KUBAKI MPAKA MWISHO....!!!!

No comments:

Post a Comment