Wednesday, April 6, 2011

Ndege ya Raisi yatunguliwa kwa risasi Rwanda siku kama ya leo.....

1994 - Aprili 6, ndege ya Rais Habyarimana ilipigwa risasi ikiwa angani kabla ya kutua na kutodondoshwa chini. Yeye na Rais wa Burundi wakauawa, lawama zote zikapelekwa kwa Watutsi, wakaanzisha Mauaji ya alaiki. Picha inaonyesha mwanajeshi akiangalia MABAKI ya ndege alimokuwawo raisi


miaka 17 iliyopita leo, wanaume na wanawake, watoto na watu wazima, walitapakaa katika mitaa ya miji kama Kigali na kunyongwa katika molekuli.


Siku iliyofuata FAR na Interahamwe wakasimama barabarani na kuuwa mamilioni ya watu kwa mapanga, wanawake na watoto wakabakwa na wengine kuteswa huku ndugu zao wakishuhudia.

Sababu ya kudai mgawanyo wa MADARAKA ambao Raisi Habyarimana alikuwa akiuchelewesha


wengi wakakimbia mji wao kunusuru uhai wa maisha

Inakadiriwa takribani maraia 800,000 na 1,071,000 waliuawa wakiwamo watusi na wahutu wenye msimamo wa wastani

baada ya wiki moja tu baada ya ndege ya raisi kutunguliwa mambo yalikuwa kama hivi, hapa ni ktk moja ya makanisa ambapo mauaji yalifanyika.....


LEO HII WATU WANAPOOMBA AMANI TUNAOMBA TUKUBALIANE MAPEMA WADAU
ILI KUEPUKA MAUJA KAMA YALE YA KIMBARI

ONE LOVE AFRICA

No comments:

Post a Comment