Tuesday, May 10, 2011

Hakuna mchekeshaji mkali zaidi ya MZEE MAJUTO bongo.......!

Ktk kinyang'anyiro cha kutafuta mkali wa kuchekesha "the comedy" King Majuto aka Pedeshee Majuto ameibuka mshindi na kuwabwaga vijana wanaochekesha ktk tasnia hio.

Amri Athuman' King Majuto' alizaliwa mwaka 1948 jijini Tanga na kusoma shule Msambwini, Tanga, alianza kuigiza 1958 akiwa na umri wa miaka 9 akiigiza katika majukwaa Mzee Majuto maarufu kama King Majato ni mtunzi, muigizaji,mwandishi wa mswada.

Na ndiye muigizaji wa kwanza kuandaa kazi zake katika mikanda na kuuza akiwa na Tanzania Film Company ( TFC) Kwa sasa King Majuto ni mwigizaji mwenye mashabiki wengi kutokana maonyesho mbalimbali, vichekesho vyake aliyoshiriki nchi mbalimbali.

Mzee Majuto msanii mkongwe wa maigizo hapa nchini ameshika nafasi ya 1 na kujizolea kitita cha Tshs. 1,000,000/= ktk mashindano yaliyofanyika ukumbi wa Mango Garden Kinondoni ambapo mashabiki ndio waliokuwa majaji.

[Joti+crop.jpg]
Joti alishika nafasi ya 2 na kuzawadiwa Tshs. 800,000/=

Kingwendu nafasi ya 3 na kujinyakulia Tshs. 500,000/=

Masele cha pombe alisimama ktk nafasi ya 4 na zawadi ya Tshs. 250,000/=


Masanja alitupwa hadi nafasi ya nne na kuambulia Tshs. 150,000/=

No comments:

Post a Comment