Monday, April 16, 2012

New Sound; ANAPITA - "BARUA KWA MAMA"

Anapita, msanii wa miondoko ya AfroFusion anayewakilisha chuga kaskazini mwa Tz,sasa aja na "barua kwa mama" alorekodi pande za noizmekah.com kwa defxtro,

amesema "wimbo huu nimeuandika kutokana na maisha ya mjini jinsi yalivyo, vijana wengi tumekuja kutafuta na mama zetu wako mbali na sisi, kwa jinsi maisha yalivyo wakati mwingine mshiko wa kumpigia mother hauna, na wakati mwingine mama mwenyewe kijijini hana simu mpaka kwa jirani,kuna wakati hawa wamama hudhani kwamba tumewasahu halafu huku mjini tunakula bata lakini si kweli, ni utaftaji hapa na pale changanyia na panda shuka ya  gharama halisi ya maisha, pia kuna marafiki ambao kwa bahati mbaya mama zao washatangulia mbele za haki, nao hufikiria kuandika barua.
Nawapenda mama zetu wote duniani kwasababu natambua umuhimu wao".

Amani tele...

KUSKIZA au KU-Download HIO NGOMA Bofya MAKAVULIVE PLAYLIST HAPO JUU

No comments:

Post a Comment