MWILI wa aliyekuwa mwanzilishi wa kundi la Tip Top Connection, Abdul
TaleTale (Abdu Bonge), unatarajiwa kuzikwa leo kijijini kwao Mkuyuni
mkoani Morogoro.
Abdul Bonge anadaiwa alifikwa na umauti Machi 28 alipokuwa akikimbizwa katika
Hospitali ya Mwananyamala muda mfupi baada ya kusukumwa na kuanguka
alipokuwa akiamulia ugomvi wa vijana karibu na nyumbani kwao Magomeni,
Kagera.
Wasanii mbalimbali waliowahi kufanyakazi na Abdu Bonge enzi
za uhai wake walimsifia kuwa na moyo wa kuendeleza muziki hasa wa kizazi
kipya na pia alikuwa msikivu kwa wasanii hata kipindi alichoamua
kumuachia shughuli zote za usimamizi wa wasanii mdogo wake, Babu Tale.
Marehemu Abdul Bonge atakumbukwa kwa kazi yake nzuri ya kuwaibua wasanii
mbalimbali wa muziki wa Bongo Fleva wakiwemo Madee, MB Dog, PNC, Pingu
na Deso, Keysha, Tunda Man na Z Anto.
MBELE YAKO NYUMA YETU.....PUMZIKA KWA AMANI KAKA!!
No comments:
Post a Comment