Mkurugenzi
wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza (katikati)
akizungumza na Waandishi wa Habari leo wakati wa kutangaza kuifungulia
kampuni ya Lino International Agency kuendesha shindano la Miss
Tanzania. Kushoto ni Mkurugenzi wa Lino, Hashim Lundenga.
Awali Serikali ya Tanzania iliyafungia kwa
miaka miwili mashindano ya Miss Tanzania baada ya waandalizi kudaiwa
kukiuka taratibu na kanuni.
Mashindano hayo yaliofunguliwa mwaka
1994 yamedaiwa kuwa na upendeleo mbali na rushwa kulingana na
malalamishi yaliotolewa na wananchi pamoja na washiriki.
Kwa
mujibu wa kaimu katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa nchini Tanzania
Basata , Godfrey Mngereza,kamati ya miss Tanzania ilikiuka kanuni na
taratibu zinazoongoza mashindano hayo.
No comments:
Post a Comment