Friday, November 13, 2015

"MUZIKI WA TZ UNAKUFA GRADUALLY...." - NIKKI MBISHI

Kupitia mtandao wake wa kijamii msanii wa Hiphop Tz Nikki Mbishi Baba Malcom ametoa yake ya moyoni juu ya muziki wa Tz

 Mawazo/Maoni Yangu:
Obviously kwa utafiti wangu mdogo naweza kusema muziki wetu wa Tz unakufa gradually na wale wanaojiita wadau wanajua hilo ila kwa kuwa washachukua vyao mapema na watu wao basi hakuna namna zaidi kufunga na kufanya maombi tu.

Muziki umekuwa kama kitu cha kifamilia,yaani kama sio mwanafamilia kupata nafasi kwenye nyanja yoyote itabaki ndoto kwenye career yako hata uwe una uwezo wa Nabii Mussa.


Huwa najiuliza hivi,kama wadau wameweza kuwabrand wasanii watano Tz nzima wakafika hatua fulani kisanaa,kwanini wanashindwa kubrand wasanii 100 ambapo uwezo huo wanao kupitia patnerships zao walizonazo na makampuni makubwa.


Tz imelaaniwa kwenye sekta ya sanaa,michezo na burudani wanaojiita wadau hawana hata aibu kujifanya wanajivunia mafanikio.


Msanii gani Tz amesainiwa na Label kubwa Duniani ukimtoa Rose Mhando?
Tz ni kujuana kwingi kuliko kuweka professions mbele,kila fursa inatumika kunufaisha wachache na kukandamiza wengi,kitu kinachopelelea hata baadhi ya wanahiphop wanaojiita wanaharakati kuwa WANAFIKI wa kutupa wakiofia watapotezwa kwenye game au kukosa vijisenti vya wao kutamba mjini na mnawajua hao watu.


Msanii mwenye recognition na reputation kubwa anatengeneza project nzuri ambayo ni feasible na reasonable,anakwenda kupropose for sponsorship kwenye kampuni fulani anazungushwa mpaka anajuta kuwa msanii ili hali tunawafahamu watu ambao hata wakiandaa show vichochoroni wanadhaminiwa na makampuni makubwa licha ya ubovu wa contents zao.
Itaendelea....

 https://www.facebook.com/nikki.babamalcom?fref=n

No comments:

Post a Comment