Wednesday, June 1, 2016

MISS CHANG'OMBE 2016 INATAMBULISHWA KESHO 'MPOAFRIKA' - DAVIS CORNER

KAMPUNI ya SG Entertaiment imewataka warembo kutoka kata zote zilizopo chini ya chang'ombe wenye sifa na vigezo stahiki kujitokeza bila kuogopa  kuchukua fomu za kushindani wa Miss Chang'ombe.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa mashindano hayo Adam Hussein,  alisema uzinduzi wa uchukuaji fomu hizo zitaanza kuchukuliwa kesho kutwa  saa 2:00 asubhi na kutarajiwa kuisha Juni 5 mwaka huu eneo la CDS Park (TCC Club) Chang'ombe, Mpo Afrika Davis Kona na duka la nguo la Chilu Latest Wear.

Mratibu wa Mashindano ya Shindano la Miss Chang'ombe, Adam Hussein, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusiana na kutaka Kuzinduliwa kwa Mashindano ya Urembo Miss Chang’ombe Juni 2 Mwaka huu. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano katika Shindano hilo, Victor Mkumbo
"Miss chang'ombe rasmi itazinduliwa,kesho katika ukumbi wa Mpo Afrika uliopo Davis Corner Tandika, hivyo tunaomba mtupe ushirikiano kuja kushiriki ili kuweza kukuza tasnia hii ya urembo" alisema Hussein.


Mkuu wa kutengo cha habari kutoka kampuni hiyo Victor Mkumbo, alisema vigezo vinavyotakiwa kwa washiriki hao ni kuwa na cheti cha kuzaliwa au kadi ya kupigia kura, kitambulisho cha taifa ili kuweza kuepusha udanganyifu unaojitokeza mara kwa mara.
"Baadhi ya washiriki watakao shiriki ni Neema Ogote(20), sitizuhura Husein (20), Hadija Salumu(18), Anitha Mugisha (19), Dorothea Shayo (20), Anba Mtua(20), Rehema Mongi (21), na Esther  Mnahi(22), kutoka Wilayani Temeke" alisema.

Alisema fainali ya mashindano hayo yatafanyika Julai 21 mwaka huu katika viwanja vya CDS Park, ambavyo zamani vilijuwa vikitwa TCC Club Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo utasindikizwa na wasanii kibao akiwepo MSAGA SUMU, CHEMICAL, GALATONE na wasanii wengine Kibao huku mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Diwani wa Kata ya Tandika 

No comments:

Post a Comment