Friday, April 19, 2013

Bomba Fm Mbeya imetangaza mchongo wa Utangazaji.........

Kituo cha Bomba Fm Mbeya kimetangza ajira moja katika kituo hicho, ambapo mmoja kati ya watu watakao kuwa wakiwania nafasi hiyo ya ajira watashindana moja kwa moja kupitia vipindi viwili.

Akitangaza nafasi hiyo wakati wa kipindi cha Kali za Bomba kinachorushwa hewani Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 7 ya mchana hadi saa 10 ya jioni, Meneja Mkuu wa Kituo hicho FREDY HELBERT amesema licha ya ajira hiyo kutolewa kupitia mashindano bado vigezo na taratibu za kazi zitazingatiwa.

Mshindi wa mashindano atapatikana kwa ushirikiano mkubwa kati yake na wasilikilizaji ambao ndio watakuwa majaji wakuu……

VIGEZO vya mshiriki:-
1. Awe na umri wa kuanzia miaka 18.
2. Awe raia wa Tanzania.
3. Awe na elimu ya kuanzia Kidato cha nne.
4. Awe hana mkataba wowote na kampuni yoyote ile.
5. Awe hajawahi kufungwa jela au kushitakiwa na kosa lolote.
6. Awe na akili timamu.
Fomu ya ushiriki ni shilingi 10,000/= tu ya Kitanzania.
Kwa Waliopo nje ya Mbeya maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia simu ya mkononi.+255764 240 440

1 comment:

  1. ACHENI UBOYA 10000 KWANI NINAKUJA KUTOA POSA HEBU ACHENI RUSHWA HIYO NI KAZI KAMA KAZI NYINGINE...

    ReplyDelete