Monday, January 26, 2015

MAWAZIRI WA AFYA WAKUTANA NA WATANZANIA - UJERUMANI

Waziri wa afya na ustawi wa jamii wa Jamuhuri ya muungano Mhe.Bw.Seif Rashid na waziri wa afya wa Zanzibar Mhe. Rashid Seif Suleiman, Siku ya jumapili 25 januari 2015 (jana) walikutana na kuongea na baadhi ya watanzania waishio nchini ujerumani katika hoteli ya Martim Hotel mjini Berlin.
 
waziri wa afya mhe.Seif Rashid (mwenye miwani) akiteta na watanzania ujerumani,mwenye kofia mwanamuziki Ebrahim Makunnja aka kamanda Ras makunja
Mawaziri hao kwa pamoja waliongozana na  balozi Tanzania nchini Ujerumani mheshimiwa Bw.Philip Malmo,katika mkutano huo mawaziri hao wote walielezea jinsi wizara zao zinavyofanya kazi kuhakikisha kuwa huduma za afya zinawafakia walio wengi na pia kuhakikisha siku za usoni kila mtanzania atatanufahika na uduma hizo kwa kutumia bima ya afya bila kujali tofouti za uwezo wa vipato vyao. 
 
Watanzania waishio ujerumani wamefarajika sana na mkutano huo,pia mawaziri wamewataka watanzania waishio ughaibuni  kuchangia kuwekeza
katika sekta ya huduma ya afya hata ikiwa ni sekta binafsi ,mawaziri hao wamesema milango ya wizara zao hipo wazi kwa watanzania wanaotaka ushauri,ushirikiano au kuwekeza katika sekta hizo.

No comments:

Post a Comment